
Novemba ni Mwezi wa Biblia Duniani
Neno la Mungu lilibadilisha historia. Liruhusu likubadilishe wewe pia
Neno la Mungu linapogusa maisha ya watu, huwabadilisha. Na watu waliobadilishwa na Neno hubadilisha ulimwengu
Novemba hii, Tumia muda zaidi kusoma Neno la Mungu na uone kitakachotokea. Tafiti zinaonyesha kwamba kuwa na desturi ya kusoma Biblia mara kwa mara kunaweza kubadilisha kila kitu. Jiunge na watu kutoka kote duniani—watu binafsi, huduma mbali mbali, kampuni tofauti za kimataifa na programu za Biblia, yaani Bible apps —tunapoungana kutumia siku 30 mfululizo katika Neno la Mungu kupitia Mpango wa Siku 30 wa Kusoma Biblia.

Je, uko tayari?
Tenga muda wa kusoma na kutafakari Neno la Mungu kwa siku 30 mfululizo kupitia Mpango wa Siku 30 wa Kusoma Biblia.
Jiunge Nasi- Sherehekea Biblia
- Tumia siku 30 katika Neno la Mungu
- Jiunge na harakati ya kimataifa ya Biblia
- Pokea barua pepe za kutia moyo
Je, wewe ni kanisa?
Toa ujumbe au mfululizo wa ujumbe kuhusu jinsi Neno la Mungu linavyobadilisha maisha wakati wa Novemba, na uhimize kanisa lako kufungua Neno la Mungu kwa siku 30 mfululizo kupitia Mpango wa Siku 30 wa Kusoma Biblia.
Sajili Kanisa LanguJe, wewe ni huduma ya kikristo?
Himiza watu unaowafikia ama jamii yako kusoma Neno la Mungu kwa siku 30 mfululizo kupitia Mpango wa Siku 30 wa Kusoma Biblia.
Sajili Huduma Yangu ya Kanisa